Jumanne, Desemba 09, 2014

Msaidizi wa kazi za ndani (hausigeli), Rehema Ally (17), mkazi wa Yombo, Machimbo Mwisho, Ilala jijini Dar, amechanwachanwa kwa wembe na kisu sehemu mbalimbali za mwili wake, hali iliyosababisha alazwe katika Hospitali ya Amana kwa matibabu.

Akizungumza na Uwazi nyumbani kwa mwajiri wake aliyejulikana kwa jina moja la Ghati, Yombo jijini Dar, Rehema aliyefika jijini hapa Januari, 2013 akitokea nyumbani kwao, Masasi mkoani Mtwara, alikuwa na haya ya kusema:

“Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni Jumapili ya Novemba 30, saa moja usiku nikiwa nje ya nyumba ya bosi wangu. Akatokea msichana mmoja aitwaye Fatuma na mwenzake aitwaye Ashura huku wakiwa wamebeba kisu na wembe. Wakanikamata kwa nguvu na kunikaba, wakaniangusha chini na kuanza kunichanachana mwili mzima.

 Rehema Ally akiwa na majeraha mwilini mwake baada ya kujeruhiwa.

“Wakati huo nilikuwa naelekea nyumbani kwa akina Fatuma kuchukua sanduku langu ambalo alilichukua kwa bosi wangu akidai kwamba nimempotezea ‘memori kadi’ ya simu yake hivyo alisema kwamba mpaka nitakapomrudishia ndipo nitakapochukua sanduku langu.

Rehema Ally akionyesha moja ya jeraha alilopata mkononi.

0 comments:

Chapisha Maoni