Jumatatu, Januari 20, 2014


LICHA ya umri kumtupa mkono, mkongwe wa sanaa ya maigizo Bongo, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’ amewastaajabisha mashabiki wake baada ya kunaswa akiwa amebandika kope za bandia.


Tukio hilo lilijiri juzikati jijini Dar wakati staa huyo alipokuwa katika harakati za hapa na pale ndipo paparazi wetu alipomshtukia na kumtandika picha kadhaa kisha kumuuliza, kulikoni?

“Hahaha! Jamani hebu mniache kidogo na mimi nataka niende na wakati kwanza ni vigumu kunibaini kama nimeweka kope hizi hasa ukiwa siyo mfuatiliaji wa mambo haya,” alisema Bi. Mwenda.

0 comments:

Chapisha Maoni