Jumamosi, Januari 25, 2014


Mabingwa Watetezi, Bayern Munich, ambao pia ndio Vinara wa ligi hiyo leo wametembeza kichapo cha bao 2-0 kwa timu ya Borussia Monchengladbach.


Timu hizo Borussia Monchengladbach na Bayern Munich ni baada ya kurejea tena kwa Ligi hiyo tangu kabla ya Christmass, Borussia Monchengladbach inayoshika nafasi ya 3 kwenye msimamo ikiwa na alama 33 pointi 11 nyuma ya vinara hao sasa zimeongezeka kwa kukubali kichapo kutoka kwa timu ya Bayern Munich bao 2-0, Bao zikifungwa na Mario Götze katika dakika ya 7 huku bao la pili likifungwa kipindi cha pili kwa mkwaju wa penati na Thomas Müller katika dakika ya 53.


0 comments:

Chapisha Maoni