Jumamosi, Februari 01, 2014

Tahadhari kuhusu mbinu mpya ya kutapeliwa fedha ukitoka kwenye ATM

Matapeli wamebuni mbinu mpya ya kuibia watu fedha punde wanapotoka kuzichukua kwenye ATM.

Punde unapomaliza kuchukua fedha, anakuja mtu anakuomba msaada wa chenji kwa kuwa naye amechukua fedha ila imempa noti kubwa tu.

Huruma na wema wako wa kutoa chenji unasababisha akupe noti zisizo halali (fake bills) na wewe unakuwa ulishampatia zilizo halali.

Pichani ni mojawapo ya tukio halisi lililomtokea mtu ambaye ameamua kuwashirikisha wengine ili wajihadhari.

Alikumbwa na utapeli huo alipochukua fedha katika maeneo ya CBE, Dar es Salaam.

Jihadhari!

0 comments:

Chapisha Maoni