Alhamisi, Januari 23, 2014


Mashuhuda walisema waliona maiti ya mtu ikielea kwenye maji yaliyokuwa yakipita kwa kasi, tukio ambalo lilithibitishwa na Diwani wa Kata ya Magole, Juma Rajabu Chewe. Chewe alisema maiti hiyo ilionekana ikielea eneo la Mateteni na kwamba taarifa zilitolewa polisi ili aopolewe. Hadi jana jioni idadi ya watu walioathiriwa na maafa ilikuwa bado haijafahamika.

Maji yasambaa kwenye vijiji mbalimbali vinavyozunguka mto huo na kuwalazimisha baadhi ya watu kulazimika kujiokoa kwa kupanda kwenye paa za nyumba zao huku wengine wakikwea juu ya miti.

Baadhi ya watu walikutwa na mafuriko hayo mashambani na walipozidiwa na nguvu ya maji walijiokoa kwa kushikilia vitu mbalimbali ikiwamo miti, huku baadhi yao wakipoteza nguo walizokuwa wamevaa walipokuwa kwenye harakati za kujiokoa.

Polisi waliofika eneo hilo kwa ajili ya uokoaji walilazimika kuomba helikopta kutoka makao makuu ya jeshi hilo, Dar es Salaam ili kuwaokoa watu waliokuwa kwenye paa za nyumba na kwenye miti iliyokuwa imezungukwa na maji.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera alitaka kuwapo kwa uvumilivu wakati Serikali ikiendelea na taratibu za kuwaokoa walioko juu ya miti na kutoa misaada kwa walioathirika.

Alisema kuwa kutokana na hali kuwa mbaya, ofisi yake ililazimika kuomba helikopta kwa ajili ya kuongeza nguvu ya juhudi za uokoaji.

Taharuki kubwa
Mafuriko hayo yalizua taharuki kubwa kiasi cha wananchi kutawanyika ovyo wakiwa hawajui cha kufanya, kutokana na nyumba zao kuharibiwa na mali zao hususan mazao yakisombwa na maji.

Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa kina mama wakiwa na watoto ambao walionekana katika makundi wakiomba msaada baada ya kukimbia makazi yao, huku wengi wakiwa wamelowa kutokana na kunyeshewa.


Kutazama picha za daraja hilo lililovunjika BOFYA HAPA

0 comments:

Chapisha Maoni