MAMIA ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), asubuhi ya leo wamejitokeza kumsindikiza Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Freeman Mbowe kuelekea Makao Makuu ya Jeshi la Polisi yaliyopo Posta jijini Dar es Salaam.
Ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa eneo la Makao Makuu ya Polisi wakati Freeman Mbowe akiwasili kuhojiwa.
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema Taifa (Bawacha), Halima Mdee akiwasili Makao Makuu ya Polisi jijini Dar leo.
Wananchi wakiwa Makao Makuu ya Polisi.
Mbowe amefika makao makuu hayo kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu kauli yake aliyoitoa Jumapili iliyopita ya kuitisha maandamano nchi nzima kushinikiza kusitishwa kwa Bunge Maalumu la Katiba.
Katika tukio hilo, baadhi ya waandishi wa habari wamekimbizwa na polisi waliokuwa na mbwa wakitakiwa kukaa umbali wa mita 200 kutoka katika makao makuu hayo ya polisi.




0 comments:
Chapisha Maoni