Alhamisi, Mei 15, 2014

Tairi ya bajaji  hiyo  likiwa  limekatika.

 Askari  wa usalama  barabara  wakikagua ajali  hiyo iliyosababisha hadi ukuta wa uzio wa bustani ya  Manispaa ya Iringa  kubomoka.

 Bajaji  ikiwa  imepata  ajali mchana  huu eneo la posta mjini Iringa.

 Bajaji ya Mng'aro  wa sembe  akiwa emepata ajali  wakati ikisambaza unga  huo.

 Wananchi  wakishuhudia ajali  hiyo mbaya.





 Maneno  ya maudhi yaliyoa ndikwa nyuma ya Bajaji 'FUATA YAKO" nusuru  yamtokee  puani dereva

BINTI mmoja  ambae ni  mwanafunzi wa  shule ya  Sekondari mjini Iringa amejeruhiwa  vibaya baada ya  kugongwa na Bajaji ya kampuni ya unga ya Mng'aro wa Sembe  ya mjini hapa.

Ajali  hiyo  imetokea majira ya saa 8.35 mchana  wa  leo  katika eneo la Posta barabara ya  Iringa- Dodoma wakati  Bajaji  hiyo ikitokea  eneo la Kihesa kuja mjini Iringa.

Mashuhuda  wa ajali  hiyo  wameueleza mtandao  huu kuwa chanzo  cha ajali  hiyo ni  mwendo kasi ambao dereva wa bajaji .

Kwani  alisema iwapo  dereva  huyo angekuwa katika mwendo wa kawaida  ajali  hiyo  isingetokea.

Hata  hivyo  mashuhuda hao akiwemo Bw Mashaka Kayoka  ambae ni mmoja kati ya wauza magazeti  maaarufu  eneo hilo la posta alisema  kuwa binti  huyo ni mtu pekee aliyejeruhiwa japo  eneo hilo huwa wanashinda  watu  wenye ulemavu wa  viongo wakijishughulisha kwa biashara ila  wamenusurika  .

Mbali ya  mwanafunzi huyo kujeruhiwa hakuna mtu mwingine  aliyejeruhiwa na dereva wa  bajaji  hiyo amekamatwa .

0 comments:

Chapisha Maoni